zaidi ya mbuzi na kondoo 200 huko morogoro wilaya ya mvomero kijiji cha dihinda wamekatwa katwa na walinzi wa jadi kutoka Gairo wanaojulikana kwa jina la Mwanu
Taarifa zinasema kuwa mifugo hiyo ilikula nusu hekari ya mazao ya mkulima mmoja kijijini hapo na taarifa ziliwafikia walinzi hao ambapo walifika na kukatakata hiyo mali ya mama mmoja mjane mfugaji wa jamii ya kimasai
Lakini inadaiwa kuwa mifugo ya mama huyo haikuhusuka kula mazao hayo bali ni mifugo ya mfugaji mwingine ndio iliyohusika
waziri mwenye dhamana kupitia wizara ya mifugo na kilimo hivi sasa ameelekea eneo la tukio
Post a Comment