Featured

    Featured

  • Shukrani kwa kutembelea mtandao huu
  • Sambaza mtandao huu kadri uwezavyo
  • Tangaza nasi kwa bei poa
  • Wasiliana nasi
  • Mtaanikwetublog@gmail.com
  • Shukrani

Picha ya mwigulu nchemba na mwanae yazua mjadala mitandaoni

Picha ya waziri wa kilimo na mifugo na mbunge wa Iramba Masharili Imezua "Hisia" Tofauti na mijadala mitandaoni. Picha hiyo inamuonyesha mwigulu nchemba akiwa na mwanae wa kiume na 'Caption' ya picha inayosomeka elimuniufunguo Kikubwa kilichozua mjadala ni nembo  katika fulana ya mtoto yenye maandishi ya FEZA SCHOOL.

Maswali na mijadala ya wengi ni kuwa, Itakuwaje na moyo wa kuimarisha  elimu katika shule za umma kama sehemu ya mawaziri  ambao ni watekelezaji wa sera ya elimu bure na uboreshaji wa elimu katika shule za umma wana kimbiza watoto wao katika shule binafsi?Kwanini mawaziri ambao ni sehemu ya utekelezaji wa sera wanaoamini katika elimu bora katika shule za umma wao hawawapeleki watoto wao huko?

Picha hii imezua mijadala tofauti tofauti na wapo wanaoona Mh. Mwigulu yupo sahihi  kupeleka watoto shule binafsi sababu ukweli ni kuwa shule za serikali elimu yao ni duni na isiyo na ushindani.

Hivyo mawaziri kuwapeleka watoto wao shule binafsi na  zenye ubora kama FEZA SCHOOL ni kuwaepusha na elimu duni inayotolewa na serikali


Toa maoni yako hapo chini

author

Author Name

Author Description!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

www.CodeNirvana.in

Translate

Total Pageviews

Copyright © Mtaani Kwetu | Designed By Balozi wa mtaa